Wagalatia 1:21-24 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.

22. Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.

23. Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: “Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza.”

24. Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

Wagalatia 1