Waefeso 5:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. (

29. Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,

30. maana sisi ni viungo vya mwili wake).

31. “Kwa sababu hiyo, mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”

Waefeso 5