Waefeso 5:11-16 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Msishiriki katika matendo yasiyofaa ya giza, bali yafichueni.

12. Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.

13. Lakini kila kitu kikifichuliwa na mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;

14. na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema:“Amka wewe uliyelala,fufuka kutoka kwa wafu,naye Kristo atakuangaza.”

15. Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi. Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.

16. Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.

Waefeso 5