Waebrania 4:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”

5. Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.”

6. Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii.

7. Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa:“Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,msiwe wakaidi.”

8. Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.

Waebrania 4