Waebrania 11:20-24 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.

21. Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea kichwa cha ile fimbo yake.

22. Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.

23. Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.

24. Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.

Waebrania 11