Waebrania 10:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.

5. Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu:“Hukutaka tambiko wala sadaka,lakini umenitayarishia mwili.

6. Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.

7. Hapo nikasema:‘Niko hapa, ee Mungu, kutimiza matakwa yakokama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha sheria.’”

8. Kwanza alisema: “Hutaki wala hupendezwi na tambiko, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi.” Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na sheria.

Waebrania 10