35. Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatia tuzo kubwa.
36. Mnahitaji kuwa na uvumilivu ili muweze kutimiza matakwa ya Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37. Maana kama yasemavyo Maandiko:“Bado kidogo tu,na yule anayekuja, atakuja,wala hatakawia.
38. Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi;walakini akirudi nyuma,mimi sitapendezwa naye.”
39. Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tumo na wale wanaoamini na kuokolewa.