Waebrania 10:35-39 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatia tuzo kubwa.

36. Mnahitaji kuwa na uvumilivu ili muweze kutimiza matakwa ya Mungu na kupokea kile alichoahidi.

37. Maana kama yasemavyo Maandiko:“Bado kidogo tu,na yule anayekuja, atakuja,wala hatakawia.

38. Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi;walakini akirudi nyuma,mimi sitapendezwa naye.”

39. Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tumo na wale wanaoamini na kuokolewa.

Waebrania 10