7. Samsoni akawaambia hao Wafilisti, “Kama hayo ndiyo mliyoyafanya, naapa kwamba sitaondoka mpaka nimelipiza kisasi.”
8. Basi, akawashambulia vikali na kuwaua wengi. Kisha akaenda kuishi katika pango la mwamba wa Etamu.
9. Wafilisti wakaja, wakapiga kambi yao nchini Yuda na kuushambulia mji wa Lehi.