Mwanzo 47:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, Yosefu akaenda kwa Farao, akamwambia, “Baba yangu na ndugu zangu pamoja na kondoo, ng'ombe na mali yao yote, wamefika kutoka nchi ya Kanaani. Sasa wako katika eneo la Gosheni.”

2. Yosefu alikuwa amewachukua ndugu zake watano, akawajulisha kwa Farao.

3. Farao akawauliza, “Kazi yenu ni nini?” Wakamjibu, “Bwana, sisi watumishi wako ni wachungaji, kama walivyokuwa babu zetu.”

Mwanzo 47