20. Huko Misri, Asenathi, binti Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efraimu.
21. Wana wa Benyamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
22. Watu hao kumi na wanne ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Raheli, mkewe.
23. Dani na Hushimu, mwanawe.
24. Naftali na wanawe: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
25. Hao saba ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Bilha, mjakazi ambaye Labani alimpa binti yake Raheli.