21. Baadaye akazaa mtoto wa kike, akamwita Dina.
22. Kisha Mungu akamkumbuka Raheli, akalikubali ombi lake na kumjalia kupata watoto.
23. Raheli akapata mimba, akajifungua mtoto wa kiume, akasema, “Mungu ameniondolea aibu yangu.”
24. Kwa hiyo akamwita mtoto huyo Yosefu akisema, “Mwenyezi-Mungu na aniongezee mtoto mwingine wa kiume.”
25. Baada ya Raheli kumzaa Yosefu, Yakobo akamwambia Labani, “Niruhusu nirudi nyumbani, katika nchi yangu.