18. Ardhi itakuzalia michongoma na magugu,nawe itakubidi kula majani ya shambani.
19. Kwa jasho lako utajipatia chakulampaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa;maana wewe ni mavumbi, na mavumbini utarudi.”
20. Adamu akampa mkewe jina “Hawa”, kwani alikuwa mama wa binadamu wote.
21. Mwenyezi-Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
22. Kisha Mwenyezi-Mungu akasema, “Sasa, binadamu amekuwa kama mmoja wetu, anajua mema na mabaya. Lazima kumzuia kula lile tunda la mti wa uhai, kwani akilila ataishi milele!”