Mwanzo 25:7-9 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Abrahamu aliishi miaka 175.

8. Alifariki baada ya kuishi maisha marefu na ya fanaka, akajiunga na wazee wake waliomtangulia.

9. Isaka na Ishmaeli, wanawe Abrahamu, wakamzika baba yao katika pango la Makpela, mashariki ya Mamre kwenye shamba lililokuwa la Efroni, mwana wa Sohari, Mhiti.

Mwanzo 25