Mwanzo 17:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Nami nitafanya agano nawe na kuwazidisha wazawa wako.”

3. Hapo Abramu akasujudu. Naye Mungu akamwambia,

4. “Ninafanya agano hili nawe: Utakuwa baba wa mataifa mengi.

5. Tangu sasa, hutaitwa tena Abramu, bali utaitwa Abrahamu, maana nimekufanya kuwa baba wa mataifa mengi.

6. Nitakufanya uwe na wazawa wengi sana; kwako nitazusha mataifa mengi na wafalme.

Mwanzo 17