2. Nami nitafanya agano nawe na kuwazidisha wazawa wako.”
3. Hapo Abramu akasujudu. Naye Mungu akamwambia,
4. “Ninafanya agano hili nawe: Utakuwa baba wa mataifa mengi.
5. Tangu sasa, hutaitwa tena Abramu, bali utaitwa Abrahamu, maana nimekufanya kuwa baba wa mataifa mengi.
6. Nitakufanya uwe na wazawa wengi sana; kwako nitazusha mataifa mengi na wafalme.