Mwanzo 1:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne.

20. Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.”

21. Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema.

Mwanzo 1