Mika 2:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Ninapanga kuwaleteeni nyinyi maafa,ambayo kamwe hamtaweza kuyakwepa.Utakuwa wakati mbaya kwenu,wala hamtaweza kwenda kwa maringo.

4. Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo,watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema:‘Tumeangamia kabisa;Mwenyezi-Mungu amechukua nchi yetu,naam, ameiondoa mikononi mwetu.Mashamba yetu amewagawia waliotuteka.’”

5. Kwa hiyo hamtagawiwa sehemu yoyote ya ardhimiongoni mwa watu wake Mwenyezi-Mungu.

6. “Usituhubirie sisi.Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa.Sisi hatutakumbwa na maafa!

Mika 2