6. Maana, kicheko cha mpumbavuni kama mlio wa miiba motoni.Hayo nayo ni bure kabisa.
7. Mwenye hekima akimdhulumu mtu;hujifanya mwenyewe kuwa mpumbavukupokea rushwa hupotosha akili.
8. Mwisho wa jambo ni afadhali kuliko mwanzo wake;mvumilivu rohoni ni bora kuliko mwenye majivuno.
9. Usiwe mwepesi wa hasira,maana, hasira hukaa ndani ya wapumbavu.
10. Usiulize, “Kwa nini nyakati za kale zilikuwa bora kuliko za sasa?”Huulizi hivyo kwa kutumia hekima.
11. Hekima ni ya thamani kubwa kama urithi;ni muhimu kwa wale wote walio hai.