3. Huzuni ni afadhali kuliko kichekomaana, huzuni ya uso ni faida ya moyo.
4. Moyo wa mwenye hekima huthamini matanga,lakini moyo wa mpumbavu hupenda raha.
5. Afadhali kusikia maonyo ya wenye hekimakuliko kusikiliza nyimbo za wapumbavu.
6. Maana, kicheko cha mpumbavuni kama mlio wa miiba motoni.Hayo nayo ni bure kabisa.
7. Mwenye hekima akimdhulumu mtu;hujifanya mwenyewe kuwa mpumbavukupokea rushwa hupotosha akili.
8. Mwisho wa jambo ni afadhali kuliko mwanzo wake;mvumilivu rohoni ni bora kuliko mwenye majivuno.
9. Usiwe mwepesi wa hasira,maana, hasira hukaa ndani ya wapumbavu.
10. Usiulize, “Kwa nini nyakati za kale zilikuwa bora kuliko za sasa?”Huulizi hivyo kwa kutumia hekima.
11. Hekima ni ya thamani kubwa kama urithi;ni muhimu kwa wale wote walio hai.
12. Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na fedha.Faida ya maarifa ni kwamba hekima hulinda maisha ya mtu aliye nayo.
13. Tafakarini vema kazi yake Mungu;ni nani awezaye kunyosha alichopinda Mungu?