Mhubiri 10:18-20 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Kutokana na uvivu wa mtu, paa hubonyea;kwa sababu ya uzembe, nyumba huvuja.

19. Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha,divai huchangamsha maisha;na fedha husababisha hayo yote.

20. Usimwapize mtawala hata moyoni mwako,wala usimwapize tajiri hata chumbani mwako unakolala,kwa kuwa ndege ataisikia sauti yako,au kiumbe arukaye atatangaza maneno yako.

Mhubiri 10