Methali 9:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Amechinja wanyama wa karamu,divai yake ameitayarisha,ametandika meza yake.

3. Amewatuma watumishi wake wa kike mjini,waite watu kutoka kwenye vilele vya miinuko:

4. “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:

5. “Njoo ukale chakula,na unywe divai niliyotengeneza.

6. Achana na ujinga upate kuishi;fuata njia ya akili.”

7. Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.

Methali 9