Methali 8:31-36 Biblia Habari Njema (BHN)

31. nikifurahia dunia na wakazi wake,na kupendezwa kuwa pamoja na wanadamu.

32. “Sasa basi wanangu, nisikilizeni:Heri wale wanaofuata njia zangu.

33. Sikilizeni mafunzo mpate hekima,wala msiyakatae.

34. Heri mtu anayenisikiliza,anayekaa kila siku mlangoni pangu,anayekesha karibu na milango yangu.

35. Anayenipata mimi amepata uhai,amepata upendeleo kwa Mwenyezi-Mungu.

36. Asiyenipata anajidhuru mwenyewe;wote wanaonichukia wanapenda kifo.”

Methali 8