Methali 8:19-23 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Matunda yangu ni mazuri kuliko dhahabu safi,faida yangu yashinda ile ya fedha bora.

20. Natembea katika njia ya uadilifu;ninafuata njia za haki.

21. Mimi huwatajirisha wanaonipenda,huzijaza tele hazina zao wanipendao.

22. “Mwenyezi-Mungu aliniumba mwanzoni mwa kazi yake,zama za zama kabla ya kuwako kitu chochote.

23. Nilifanywa mwanzoni mwa nyakati,nilikuwako kabla ya dunia kuanza.

Methali 8