18. Utajiri na heshima viko kwangu,mali ya kudumu na fanaka.
19. Matunda yangu ni mazuri kuliko dhahabu safi,faida yangu yashinda ile ya fedha bora.
20. Natembea katika njia ya uadilifu;ninafuata njia za haki.
21. Mimi huwatajirisha wanaonipenda,huzijaza tele hazina zao wanipendao.
22. “Mwenyezi-Mungu aliniumba mwanzoni mwa kazi yake,zama za zama kabla ya kuwako kitu chochote.