23. Hakutambua kwamba hiyo itamgharimu maisha yake,mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mshale moyoni,amekuwa kama ndege aliyenaswa wavuni.
24. Sasa wanangu, nisikilizeni;yategeeni sikio maneno ya kinywa changu.
25. Msikubali kuongozwa na mwanamke kama huyo,wala msipitepite katika mapito yake.
26. Maana amewaangusha wanaume wengi;ni wengi mno hao aliowachinja.
27. Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu,ni mahali pa kuteremkia mautini.