Methali 7:23-27 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Hakutambua kwamba hiyo itamgharimu maisha yake,mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mshale moyoni,amekuwa kama ndege aliyenaswa wavuni.

24. Sasa wanangu, nisikilizeni;yategeeni sikio maneno ya kinywa changu.

25. Msikubali kuongozwa na mwanamke kama huyo,wala msipitepite katika mapito yake.

26. Maana amewaangusha wanaume wengi;ni wengi mno hao aliowachinja.

27. Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu,ni mahali pa kuteremkia mautini.

Methali 7