Methali 6:27-34 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Je, waweza kuweka moto kifuanina nguo zako zisiungue?

28. Je, waweza kukanyaga makaa ya motona nyayo zako zisiungue?

29. Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.

30. Watu hawambezi sana mtu akiiba kwa sababu ya njaa;

31. lakini akipatikana lazima alipe mara saba;tena atatoa mali yote aliyo nayo.

32. Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa;huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.

33. Atapata majeraha na madharau;fedheha atakayopata haitamtoka.

34. Maana wivu wa mume humfanya kuwa mkali kabisa;wakati atakapolipiza kisasi hana cha kuhurumia.

Methali 6