Methali 5:21-23 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Kumbuka njia za mtu zi wazi mbele ya Mwenyezi-Mungu;yeye anaona kila hatua anayochukua binadamu.

22. Mtu mwovu hunaswa kwa uovu wake mwenyewe;hukamatwa katika tanzi za dhambi yake mwenyewe.

23. Yeye hufa kwa utovu wa nidhamu,huangamia kwa sababu ya upuuzi wake mkuu.

Methali 5