9. Atakuvika kilemba kizuri kichwani pako,atakupa taji maridadi.”
10. Mwanangu, sikia na kuyapokea maneno yangu,ili upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.
11. Nimekufundisha njia ya hekima,nimekuongoza katika njia nyofu.
12. Ukitembea hatua zako hazitazuiwa,wala ukikimbia hutajikwaa.
13. Zingatia mafundisho ya Hekima na usimwache aponyoke,mshike kwa makini maana yeye ni uhai wako.