21. Kuna mambo matatu ambayo huitetemesha dunia,naam, mambo manne ambayo haiwezi kuyastahimili:
22. Mtumwa anayekuwa mfalme;mpumbavu anayeshiba chakula;
23. mwanamke asiyependwa anayeolewa;na mjakazi achukuapo nafasi ya bibi yake.
24. Kuna viumbe vinne vidogo sana duniani,lakini vina akili sana:
25. Sisimizi: Wadudu wasio na nguvu,lakini hujihifadhia chakula wakati wa kiangazi;
26. pelele: Wanyama wasio na uwezo,lakini hujitengenezea makao miambani;