Methali 30:21-26 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Kuna mambo matatu ambayo huitetemesha dunia,naam, mambo manne ambayo haiwezi kuyastahimili:

22. Mtumwa anayekuwa mfalme;mpumbavu anayeshiba chakula;

23. mwanamke asiyependwa anayeolewa;na mjakazi achukuapo nafasi ya bibi yake.

24. Kuna viumbe vinne vidogo sana duniani,lakini vina akili sana:

25. Sisimizi: Wadudu wasio na nguvu,lakini hujihifadhia chakula wakati wa kiangazi;

26. pelele: Wanyama wasio na uwezo,lakini hujitengenezea makao miambani;

Methali 30