Methali 3:30-35 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Usigombane na mtu bila sababuikiwa hajakudhuru kwa lolote.

31. Usimwonee wivu mtu mkatili,wala usiige mwenendo wake.

32. Maana waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu;lakini yeye huwafanya marafiki zake wale walio wanyofu.

33. Mwenyezi-Mungu huapiza nyumba za waovu,lakini huyabariki makao ya waadilifu.

34. Yeye huwadharau wenye dharau,lakini huwafadhili wanyenyekevu.

35. Wenye hekima watavuna heshima,lakini wapumbavu watapata fedheha.

Methali 3