18. Pasipo maono ya kinabii watu hukosa nidhamu;heri mtu yule anayeshika sheria.
19. Mtumwa haonyeki kwa maneno matupu,maana ingawa anayaelewa yeye hatayatii.
20. Wamwona mtu apayukaye bila kufikiri?Mtu mpumbavu ni afadhali kuliko yeye.
21. Ambembelezaye mtumwa wake tangu utoto,mwishowe mtumwa huyo atamrithi.
22. Mwenye ghadhabu huchochea ugomvi,mtu wa hasira husababisha makosa mengi.
23. Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe,lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.
24. Anayeshirikiana na mwizi anajidhuru mwenyewe;husikia laana ya aliyeonewa bila kusema neno.
25. Kuwaogopa watu ni kujitega mwenyewe,lakini anayemtumaini Mwenyezi-Mungu yu salama.
26. Wengi hupenda kujipendekeza kwa mtawala,hali mtu hupata haki yake kwa Mwenyezi-Mungu.
27. Mdhalimu ni chukizo kwa mnyofu,naye mnyofu ni chukizo kwa mwovu.