15. Adhabu na maonyo huleta hekima,lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.
16. Waovu wakitawala maovu huongezeka,lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao.
17. Mpe nidhamu mwanao naye hatakupa wasiwasi;yeye ataufurahisha moyo wako.
18. Pasipo maono ya kinabii watu hukosa nidhamu;heri mtu yule anayeshika sheria.
19. Mtumwa haonyeki kwa maneno matupu,maana ingawa anayaelewa yeye hatayatii.