6. Usijipendekeze kwa mfalme,wala usijifanye mtu mkubwa,
7. maana ni heri kuambiwa, “Njoo huku mbele”,kuliko kuporomoshwa mbele ya mkuu.Mambo uliyoyaona kwa macho yako,
8. usiharakishe kuyapeleka mahakamani;maana utafanya nini hapo baadaye,shahidi mwingine akibatilisha hayo usemayo?
9. Suluhisha ugomvi na mwenzako peke yake,na kila mmoja wenu asitoe siri ya mwenzake;
10. watu wasije wakajua kuna siri,ukajiharibia jina lako daima.
11. Neno lisemwalo wakati unaofaa,ni kama nakshi za dhahabu juu ya madini ya fedha.