Methali 25:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hizi nazo ni methali nyingine za mfalme Solomoni walizonakili watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.

2. Mungu hutukuzwa kwa kuficha mambo,lakini mfalme hutukuzwa kwa yale anayoeleza.

3. Kama zilivyo mbali mbingu na kirefu kina cha ardhindivyo zisivyochunguzika akili za mfalme.

4. Toa takataka katika fedha,na mhunzi atakutengenezea chombo kizuri.

Methali 25