Methali 24:29-33 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda!Ni lazima nilipize kisasi!”

30. Nilipitia karibu na shamba la mvivu;shamba la mzabibu la mtu mpumbavu.

31. Nilishangaa kuona limemea miiba,magugu yamefunika eneo lake lote,na ukuta wake wa mawe umebomoka.

32. Nilitazama, nikawaza,mwishowe nikapata funzo:

33. Lala tu kidogo; sinzia tu kidogo!Kunja mikono yako tu upumzike!

Methali 24