29. Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda!Ni lazima nilipize kisasi!”
30. Nilipitia karibu na shamba la mvivu;shamba la mzabibu la mtu mpumbavu.
31. Nilishangaa kuona limemea miiba,magugu yamefunika eneo lake lote,na ukuta wake wa mawe umebomoka.
32. Nilitazama, nikawaza,mwishowe nikapata funzo:
33. Lala tu kidogo; sinzia tu kidogo!Kunja mikono yako tu upumzike!