18. maana Mwenyezi-Mungu aonaye hayo hatapendezwa;huenda akaacha kumwadhibu.
19. Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya,wala usiwaonee wivu watu waovu,
20. maana mwovu hatakuwa na mema baadaye;taa ya uhai wake itazimwa.
21. Mwanangu, umche Mwenyezi-Mungu na kumheshimu mfalme,wala usishirikiane na wale wasio na msimamo,
22. maana maangamizi yao huwapata ghafla.Hakuna ajuaye maafa watakayozusha.