Methali 23:6-9 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Usile chakula cha mtu bahili,wala usitamani mapochopocho yake,

7. maana moyoni mwake anahesabu unachokula.Atakuambia, “Kula, kunywa!”Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.

8. Utatapika vipande ulivyokula;shukrani zako zote zitakuwa za bure.

9. Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,maana atapuuza hekima ya maneno yako.

Methali 23