Methali 23:25-30 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Wafurahishe baba na mama yako;mama aliyekuzaa na afurahi.

26. Mwanangu, nisikilize kwa makini,shikilia mwenendo wa maisha yangu.

27. Malaya ni shimo refu la kutega watu;mwanamke mgeni ni kama kisima chembamba.

28. Yeye hunyemelea kama mnyanganyi,husababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.

29. Ni nani wapigao yowe?Ni nani wenye huzuni?Ni nani wenye ugomvi?Ni nani walalamikao?Ni nani wenye majeraha bila sababu?Ni nani wenye macho mekundu?

30. Ni wale ambao hawabanduki penye divai,wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.

Methali 23