Methali 21:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Shahidi mwongo ataangamia,lakini msikivu hawezi kunyamazishwa.

29. Mtu mwovu hujionesha kuwa jasiri,lakini mwadilifu huhakikisha ametenda sawa.

30. Hakuna hekima, maarifa, wala mawaidha yoyote ya mtu,yawezayo kumshinda Mwenyezi-Mungu.

31. Farasi hutayarishwa kwa vita,lakini ushindi wamtegemea Mwenyezi-Mungu.

Methali 21