28. Shahidi mwongo ataangamia,lakini msikivu hawezi kunyamazishwa.
29. Mtu mwovu hujionesha kuwa jasiri,lakini mwadilifu huhakikisha ametenda sawa.
30. Hakuna hekima, maarifa, wala mawaidha yoyote ya mtu,yawezayo kumshinda Mwenyezi-Mungu.
31. Farasi hutayarishwa kwa vita,lakini ushindi wamtegemea Mwenyezi-Mungu.