9. Ukinisikiliza utafahamu uadilifu na haki,utajua jambo lililo sawa na jema.
10. Maana hekima itaingia moyoni mwako,na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11. Busara itakulinda,ufahamu utakuhifadhi;
12. vitakuepusha na njia ya uovu,na watu wa maneno mapotovu;
13. watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;
14. watu wafurahiao kutenda maovu,na kupendezwa na upotovu wa maovu;