6. Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.
7. Maskini huchukiwa na ndugu zake;marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!Hata awabembeleze namna gani hatawapata.
8. Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake;anayezingatia busara atastawi.
9. Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa;asemaye uongo ataangamia.
10. Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.
11. Mwenye busara hakasiriki upesi;kusamehe makosa ni fahari kwake.