20. Sikiliza shauri na kupokea mafundisho,upate hekima ya kukufaa siku zijazo.
21. Kichwani mwa mtu mna mipango mingi,lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika.
22. Kinachotakiwa kwa mtu ni uaminifu;afadhali mtu maskini kuliko mtu mwongo.
23. Kumcha Mwenyezi-Mungu kunaleta uhai;amchaye hujaliwa pumziko la kutosheleza,wala hatapatwa na baa lolote.
24. Mvivu ni kama mtu atiaye mkono katika sahani ya chakula,lakini hana nguvu ya kuuinua hadi mdomoni.