Methali 19:16-23 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Anayeshika amri anasalimisha maisha yake;anayepuuza agizo atakufa.

17. Anayemsaidia maskini anamkopesha Mwenyezi-Mungu;Mwenyezi-Mungu atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao kungali bado na tumaini,lakini usimwadhibu kiasi cha kumwangamiza.

19. Mtu wa hasira kali lazima apate adhabu;ukimwachia mara moja itakubidi kumwachia tena.

20. Sikiliza shauri na kupokea mafundisho,upate hekima ya kukufaa siku zijazo.

21. Kichwani mwa mtu mna mipango mingi,lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika.

22. Kinachotakiwa kwa mtu ni uaminifu;afadhali mtu maskini kuliko mtu mwongo.

23. Kumcha Mwenyezi-Mungu kunaleta uhai;amchaye hujaliwa pumziko la kutosheleza,wala hatapatwa na baa lolote.

Methali 19