3. Ubora wa dhahabu ama fedha hupimwa kwa moto,lakini Mwenyezi-Mungu ndiye apimaye mioyo ya watu.
4. Mtenda maovu husikiliza maneno mabaya,mwongo hutegea sikio ulimi mdanganyifu.
5. Anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake;anayefurahia maafa hatakosa kuadhibiwa.
6. Wazee huwaonea fahari wajukuu zao;watoto huwaonea fahari wazazi wao.
7. Maneno mazuri si kawaida kinywani mwa mpumbavu,sembuse maneno ya uongo kinywani mwa kiongozi!
8. Kwa mhongaji, hongo ni kama hirizi;kila afanyacho hufanikiwa.
9. Anayesamehe makosa hujenga urafiki,lakini anayekumbusha makosa hutenga rafiki.