2. Mtumwa mwenye busara atachukua nafasi ya mwana mpumbavu,atapata sehemu ya urithi wa jamaa hiyo.
3. Ubora wa dhahabu ama fedha hupimwa kwa moto,lakini Mwenyezi-Mungu ndiye apimaye mioyo ya watu.
4. Mtenda maovu husikiliza maneno mabaya,mwongo hutegea sikio ulimi mdanganyifu.
5. Anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake;anayefurahia maafa hatakosa kuadhibiwa.
6. Wazee huwaonea fahari wajukuu zao;watoto huwaonea fahari wazazi wao.
7. Maneno mazuri si kawaida kinywani mwa mpumbavu,sembuse maneno ya uongo kinywani mwa kiongozi!
8. Kwa mhongaji, hongo ni kama hirizi;kila afanyacho hufanikiwa.
9. Anayesamehe makosa hujenga urafiki,lakini anayekumbusha makosa hutenga rafiki.
10. Onyo kwa mwenye busara lina maana,kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11. Afanyalo mtu mwovu ni kuasi tu;mjumbe mkatili atatumwa dhidi yake.
12. Afadhali kukutana na dubu jike aliyenyanganywa watoto wake,kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.