24. Maneno mazuri ni kama asali;ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.
25. Mtu aweza kuona njia yake kuwa sawa,lakini mwishowe humwongoza kwenye kifo.
26. Hamu ya chakula humhimiza mfanyakazi,maana njaa yake humsukuma aendelee.
27. Mtu mwovu hupanga uovu;maneno yake ni kama moto mkali.
28. Mtu mpotovu hueneza ugomvi,mfitini hutenganisha marafiki.
29. Mtu mkatili humshawishi jirani yake;humwongoza katika njia mbaya.
30. Anayekonyeza jicho kwa hila amepanga maovu;anayekaza midomo amekwisha nuia mabaya.