21. Mwenye hekima moyoni huitwa mwenye akili;neno la kupendeza huwavutia watu.
22. Hekima ni chemchemi ya uhai kwake aliye nayo,bali upumbavu ni adhabu ya wapumbavu.
23. Moyo wa mwenye hekima humwezesha kusema kwa busara;huyafanya maneno yake yawe ya kuvutia.
24. Maneno mazuri ni kama asali;ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.
25. Mtu aweza kuona njia yake kuwa sawa,lakini mwishowe humwongoza kwenye kifo.
26. Hamu ya chakula humhimiza mfanyakazi,maana njaa yake humsukuma aendelee.