16. Kupata hekima ni bora kuliko dhahabu;kupata akili ni chaguo bora kuliko fedha.
17. Njia ya wanyofu huepukana na uovu;anayechunga njia yake huhifadhi maisha yake.
18. Kiburi hutangulia maangamizi;majivuno hutangulia maanguko.
19. Afadhali kuwa mnyenyekevu na kuwa maskini,kuliko kugawana nyara na wenye kiburi.
20. Anayezingatia mafundisho atafanikiwa;heri mtu yule anayemtumainia Mwenyezi-Mungu.
21. Mwenye hekima moyoni huitwa mwenye akili;neno la kupendeza huwavutia watu.
22. Hekima ni chemchemi ya uhai kwake aliye nayo,bali upumbavu ni adhabu ya wapumbavu.
23. Moyo wa mwenye hekima humwezesha kusema kwa busara;huyafanya maneno yake yawe ya kuvutia.
24. Maneno mazuri ni kama asali;ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.
25. Mtu aweza kuona njia yake kuwa sawa,lakini mwishowe humwongoza kwenye kifo.