9. Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini Mungu huwapenda wale wafuatao mambo adili.
10. Adhabu kali ipo kwa wanaoacha mwenendo mwema;yeyote achukiaye kuonywa atakufa.
11. Ikiwa Mwenyezi-Mungu ajua yaliyo Kuzimu na Abadoni,mawazo ya binadamu yatawezaje kujificha mbele yake?
12. Mwenye madharau hapendi kuonywa,hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.
13. Moyo wa furaha hungarisha uso,lakini uchungu huvunja moyo.
14. Mwenye busara hutafuta maarifa,lakini wapumbavu hujilisha upuuzi.
15. Kwa mnyonge kila siku ni mbaya,lakini kwa mwenye moyo mchangamfu ni sikukuu.