31. Mtu ambaye husikiliza maonyo mema,anayo nafasi yake miongoni mwa wenye hekima.
32. Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe,bali anayekubali maonyo hupata busara.
33. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni shule ya hekima;kabla ya kuheshimika ni lazima kuwa mnyenyekevu.