17. Afadhali mlo wa jioni wa mchicha na upendo,kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.
18. Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi,lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.
19. Njia ya mvivu imesambaa miiba,njia ya mwaminifu ni wazi kama barabara kuu.
20. Mtoto mwenye hekima humfurahisha baba yake,lakini mpumbavu humdharau mama yake.
21. Upumbavu ni furaha kwa mtu asiye na akili,lakini mwenye busara huchagua njia iliyo sawa.
22. Mipango huharibika kwa kukosa shauri,lakini kwa washauri wengi, hufaulu.
23. Kutoa jibu sahihi hufurahisha;neno lifaalo kwa wakati wake ni jema mno!
24. Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,ili aepe kuingia chini kuzimu.
25. Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.
26. Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,bali maneno mema humfurahisha.
27. Anayetamani faida ya ulanguzianaitaabisha jamaa yake,lakini achukiaye hongo ataishi.
28. Moyo wa mwadilifu hufikiri kabla ya kujibu,lakini kinywa cha mwovu hububujika uovu.
29. Mwenyezi-Mungu yuko mbali na watu waovu,lakini yu karibu na watu wema kuwasikiliza.
30. Macho ya huruma hufurahisha moyo,habari njema huuburudisha mwili.
31. Mtu ambaye husikiliza maonyo mema,anayo nafasi yake miongoni mwa wenye hekima.
32. Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe,bali anayekubali maonyo hupata busara.
33. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni shule ya hekima;kabla ya kuheshimika ni lazima kuwa mnyenyekevu.